Thursday, August 24, 2017

HUKMU YA KUFUPISHA THANAA (KUMTUKUZA ALLAAH) NA KUMSWALIA MTUME (SWALLA ALLAAHU 'ALAYHI WA SALLAM) NA MAAMKIZI YA KIISLAM.

Image result for Hukmu Ya Kufupisha Thanaa (Kumtukuza Allaah) Na Kumswalia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) Na Maamkizi Ya Kiislam

Sifa zote njema Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wasallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Haifai kabisa kufupisha thanaa kwa maana kumtukuza Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa kuandika (s.w.t). Au kufupisha Jalla Jalaahu kwa kuandika (J.J). Vile vile haifai kumswalia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kuandika (s.a.w) au (s).

Powered by Blog - Designer