Sunday, November 6, 2016

HUKMU YA KUMLAZIMISHA MSICHANA KUOLEWA.

====================
من فتاوى فضيلة الشيخ العلامة صالح الفوزان حفظه الله.
Kutoka katika fataawa za sheikh Mwanachuoni Swaaleh Alfauzaan-Allaah amuhifadhi.
📌 السؤال :
هل للأب إجبار ابنته على الزواج؟
*Suali:*
Je inajuzu kwa Baba kumlazimisha mtoto wake wakike kuolewa?
☑️ الجواب: لا يملك الإجبار في هذا وإنما يمتنع من أن يزوجها من لا يصلح، وأما مسألة الإجبار فلا يجوز، إلا ما ذكر من أن الأب له أن يجبر البكر.
*Jawabu
Hakuna anaemiliki kulazimisha katika hili bali baba atakiwa tu akatae kumuozesha (mwanawe) Mwanamume ambaye sio mwema,
Ama mas'ala ya kulazimishana hiyo haijuzu, isipokuwa yaliyo tajwa kwamba (kuna kauli isemayo kuwa) Baba nijuu yake kumlazimisha (binti yake) bikra (katika hilo).
ولكن الصحيح خلاف هذا، وأنه ليس للأب ولا لغيره أن يجبر موليته على الزواج بمن لا تريده،
*Lakini Kauli iliyo swahihi*
(Na haki)Nikinyume na maneno hayo, Na nikwamba *Haifai kwa Baba wala mwengine yoyote kumlazimisha anaemsimamia juu ya kuolewa nimtu ambaye (labda) mwenyewe hamtaki.*
ولكن يعرض عليه ويكرر عليه وينصحها في هذا إلى أن تقتنع، فلابد أن تستشار ولا بد أن يؤخذ رأيها في هذا؛ لأن النبي صلى الله عليه وسلم: أعطى من زُوِّجَتْهُ بغير رضاها حق الفسخ.
Lakini (inayo takikana) Anamletea jambo hilo na analikariri kwake yeye na (kama hataki) anampa nasaha juu ya hilo mpaka pale atakapo kinai, Nilazima amtake ushauri na nilazima achukuwe rai yake katika hilo , Kwasababu Mtume swala na salamu zimwendee :Alimpa mwenye kuozeshwa bila ya ridhaa yake hukmu ya kuaribika ndowa.
المصدر : المنتقى من فتاوى الشيخ الفوزان (5/244)
*Chimbuko:*
Almuntaqaa min fataawaa sheikh Alfauzaan(5/244).📚.

0 comments:

Post a Comment

Powered by Blog - Designer